GENN MEDIA

KANSAS COLLEGE OF NURSING

Alhamisi, 18 Juni 2015

SAFARI YA MATUMAINI YAINGIA DOSARI LINDI BAADA YA BODABODA KUTOLIPWA MALIPO YAO KUPOKEA MSAFARA WA LOWASA

Na. Mwandishi Wetu, Lindi
Vijana waendesha pikipik(bodaba) takriba 70, mjini Lindi jana ni kama walitia doa safari ya mtangazania kupitia chama cha mapinduzi, Edward Lowassa baada ya kuchachamaa kudaia malipo waliyohaidiwa baada ya kushiriki kikamilifu mapokezi ya mtangaza nia huyo alipokuja kusaka wadhamini katika mkoa huu.
 
 
Boda Boda Lindi 
 
Wakizungumza kwa hasira baadhi ya waendesha pikipiki hao walisema hawakubali kudhulumiwa nguvu na muda wao kwa kutotimiziwa ahadi ya kulipwa fedha kwakwenda kumpokea Lowassa kutoka uwanja wa ndege wa Kikwetu hadi ofisi ya CCM mkoa wa Lindi.
"Sisi tunataka chetu maana ahadi ni deni tulikubaliana watatuwekea mafuta lita tatu kwenye pikipiki zetu na fedha taslimu shilingi elfu kumi" tena kwa muda wa saa moja tu, lakini tumekaa karibu saa saba hawataki kutulipa hawawezi kutudhulumu," alisikika kijana mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe. 
 
Akieleza kisa hicho mmoja waendesha pikipiki hao alisema wanaomunga mkono mgombea waliwahidi kuwalipa shilingi elfu kumi nakuwawekea mafuta lita tatu kila pikipiki iwapo watakwenda kumpokea ndugu Lowassa uwanja wa ndege wa kikwetu ulio nje kidogo ya manispaa ya Lindi. Nakwamba makubaliano hayo yalikuwa ni kazi ya muda wa saa moja tu. Hata hivyo walijikuta wanakaa uwanjani hapo kwazaidi ya saa saba wakimsubiri. 
 
Alisema ahadi ya kuwekewa mafuta ilitekelezwa lakini suala la fedha lilikuwa gumu baada ya mtangazania huyo kuondoka.
"kwakuwa wamekiuka makubaliano tunataka shilingi elfu thelathini maana tumekaa sana na hapa wanatupiana mpira,sasa hivi tunatoka ofisi ya CCM mkoa tunakwenda polisi,maana kuna dada mmoja ambaye ni mpambe wake tumembana yupo polisi"
 
Boda Boda Lindi 
                                                                Hali ilivyokuwa polisi.
Vijana hao waliandamana kwenda polisi, ambako walisubiri hatma ya mdai wao wakiapa hawatatoka eneo hilo hadi dada huyo awape pesa zao. Vijana hao wakiwa mbali kidogo na kituo waliendelea kubaki hadi mmoja wa askari polisi wa kituo cha Lindi alipowasihi wasifanye fujo bali wadai haki yao kwa amani.
 
"Sisi hatufanyi fujo na tumekuelewa ila tunataka haki yetu maana ni makubaliano tunataka hela yetu na sasa dau limepanda tunataka elfu arobaini," walisikika vijana hao.
Waendesha pikipiki hao waliendelea kubaki kila mmoja akipaza sauti hadi alipokwenda aliyepata kuwa mbunge wa Lindi, Abdulaziz Mohamed. Ambaye alianza kuwauliza kimetokea nini! Nao wakamjibu wanataka pesa zao.
 
"Sasa hapa polisi pana fedha zaidi ya virungu na fedha msipate! mimi simo,ondokeni na twendeni kwa utaratibu badala ya kubaki hapa," aliwaonya.
Maneno ya mbunge huyo yalionesha kuwaingia vijana hao ambao walikubali kuondoka eneo hilo na kufuata hadi kwenye nyumba ambayo hadi habari hii inaandikwa jina lake lilikuwa halijapatikana.
 
"Sasa tusikilizane fedha mtapata lakini kwa kwa utaratibu," alisema Abdulaziz.
Ndipo mbunge huyo alianza kuwaita wawakilishi kwa majina ya mahali walipotokea na kuwapatia fedha ambazo hazikuweza kufahamika ni shilingi ngapi. Ingawa taarifa za baadae ambazo zilielezwa na vijana hao kwamba walipewa shilingi elfu kuminatano kila mmoja.
"Tulikomaa hadi wakacheu mpunga,ila shilingi msimbazi na buku tano (shilingi 15000) lakini siyo mbaya," alisema kijana mwingine.
 
Dalili za hali ya hewa kuchafuka ilianza ofisi ya CCM mkoa baada ya msafara wa Lowassa kuondoka. Baada ya vijana hao kuanza kujikusanya nakuanza kuhojiana hatima ya malipo yao, huku faragha za hapa na pale zikianza kuonekana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni