Baada ya hivi karibuni kupata jina jipya
la mama cookie, staa wa bongo movies, Aunt Ezekiel amesema
amejipanga kurudi kwa kishindo kwenye bongo movies baada ya lengo lake
hilo kutimia.
Akizungumza na gazeti la Nipashe Aunt
amabaye amejifungua mwezi uluopita alisema amejipanga kutoa filamu
amabayo itahusu maswala ya wazazi ili kueleimisha wanawake wenye
tabia ya kutupu watoto wachanga mara baada ya kujifungua.
Aidha amesema huchukia wanaume wenye kuwapa mimba wanawake kisha kukataa kuhusika katika malezi ya mtoto aliyezaliwa.
Hivyo, alisema anajipanga kutoa elimu kuwa uzazi ni wakuheshimiwa na hususan kwa wanaume.
Aunt yupo katika maandalizi ya filamu hiyo ambayo atawashirikisha wasanii wakubwa na chipukizi alisema
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni