GENN MEDIA

KANSAS COLLEGE OF NURSING

Ijumaa, 19 Juni 2015

Sentensi 20 za Zitto Kabwe, Emanuel Makaidi, Ibrahim Lipumba na James Mbatia kwenye jukwaa moja la Mdahalo

DSC_4719
Swali la kwanza kabisa kuulizwa kwenye Mdahalo wa Wakuu wa Vyama waliokutanishwa jana June 18 2015 Hyatt Regency Hotel DAR, lilikuwa linahusu Changamoto ambazo wao wanaziona TZ… Alikuwepo Prof. Ibrahim Lipumba, Zitto Kabwe, James Mbatia na Emanuel Makaidi ambapo mmoja mmoja alianza kutoa majibu ya swali hilohilo.

“Nchi za Africa huwa tunabaki kulialia sana lakini lazima uangalie wenzako Duniani kuna nini… Changamoto ya kwanza ni Katiba.. pili ni rasilimali watu, changamoto nyingine ni tofauti zilizopo kati ya watu. Kuna tatizo la umaskini, lazima pia tuwafanye Watanzania wajitambue.. Kwenye sekta ya elimu hali ya Watanzania kufikiri iko chini sana”>>> James Mbatia


DSC_4689 
James Mbatia, Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi
“Katika changamoto tulizonazo iko ya mama na wajawazito, katika kila watoto 100 chini ya miaka mitano, watoto 42 wana tatizo la udumavu. Changamoto ya pili ni ukosefu wa ajira na tumeanza kuona matukio kama ya panya road, watu wamepoteza matumaini kuishi kama binadamu wa karne ya 21.
Tatizo kubwa tulilonalo ni rushwa na ufisadi, lazima tuwaweke wala rushwa wote Segerea na sio kuchukua fomu za kugombea Urais”>>> Ibrahim Lipumba.

DSC_4772
                                   Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chama cha CUF

“Ili nchi iwe sawa lazima mzawa wa Tanzania apewe nafasi ya kwanza. Changamoto nyingine ni ardhi, ardhi yetu nyingi inachukuliwa na wageni… Kingine ni Uchumi wan chi hii umedorora, ukiona fedha inapungua thamani hii ni dalili kwamba Uchumi unadorora. Changamoto nyingine ni afya, afya ya Watanzania ni mbovu. Changamoto nyingine ni elimu, hata ukienda kwenye midahalo na nchi nyingine utaona Mtanzania anapwaya” >>> Emanuel Makaidi.

DSC_4816

                                          Emanuel Makaidi, Mwenyekiti wa Chama cha NLD

“Changamoto ya kwanza tuna Uchumi usiozalisha ajira, pili tuna huduma duni za kijamii ikiwemo elimu, afya na maji… Changamoto ya tatu ni rushwa na ufisadi, changamoto ya nne ni nyufa katika nchi yetu, nyufa za udini na ukabila.. Yote haya tutayatatua kwa kuweka miiko ya Viongozi, huwezi kuwa Waziri wa Kilimo na wewe ndio una zabuni ya kusambaza Mbolea, au Waziri wa Maliasili na wewe ndio una vitalu vya kuwinda” >>> Zitto Kabwe.

DSC_4705 
                                     Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo

 Majibu yao yako kwenye hizi sauti hapa, ukipla utawasikia wote.


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni