GENN MEDIA

KANSAS COLLEGE OF NURSING

Jumanne, 16 Juni 2015

Nahreel kayasema haya kuhusu single ya ‘Nana na Nusu Nusu’ zilivyomtambulisha Afrika na kupata mafanikio

. 
Member wa kundi la Navy Kenzo ambaye pia ni mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka 2015, Nahreel amefunguka kuwa kupelekea kufanya vizuri kwa single zinazojulikana kama Nana ya Diamond Platnumz na Nusu Nusu ya Joh Makini ameanza kupata mafanikio nje ya Tanzania.
Akizungumza na millardayo.com alisema..’Kwanza nawashukuru watu kwa kunipigia kura na kuniwezesha mimi kuwa producer bora wa mwaka, na kwa upande wa kazi zipo nyingine zinakuja kuna kazi ya Joh Makini na rapper kutokea Afrika Kusini AKA, Vanessa Mdee nyingine ya Ben Pol kwa hiyo kuna kazi nyingine zinakuja kutoka nje ya Tanzania 

Tangu nilipotengeneza wimbo wa Nana ya Diamond na Nusu Nusu ya Joh Makini nimeanza kupokea connection mbalimbali kutoka Nigeria na sehemu mbalimbali kwa mfano Vanessa Mdee pia ametoka kuniambia kuwa Yemi Alade kuwa anataka kufanya kazi na mimi chini ya The Industry Studio kwa hiyo mashabiki wa Nahreel wakae tayari kwa muziki mzuri…”alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni