Nicki Minaj ni msanii wa kike ambaye tunaweza kumuweka kwenye level moja na mastaa kama akina Beyonce, uwezo wake wa kudondosha hits umefanya awe mmoja kati ya wasanii wakubwa kwenye muziki Duniani.
Kwenye moja ya Interview moja aliwahi kufanya hiki ndio alichokijibu kuhusu Lil Wayne >>> “Nasukumwa
sana na watu wanaopenda kufanya kazi, watu ambao hawatafuti sababu au
visingizio vya kutokufanya kazi… Lil Wayne namkubali sana upande wa
nidhamu yake ya kazi…sijawahi kuona! Watu wakimwona Lil Wayne wanahisi
vitu vingine lakini yule mtu yuko serious na sanaa yake na ni mmoja kati
ya wanaume wanaonisukuma sana mimi kufanya kazi hata kabla ya kuwa
chini ya Management ya Young Money“>>>
Alipoulizwa juu ya tattoo yake kwenye mkono wake wa kulia Nicki alisema >>> “Kwanza
hii tattoo ina historia ndefu sana, nilichora nikiwa na miaka 16… Baba
yangu alikasirika sana akataka kunifukuza nyumbani… Imeandikwa Kichina,
inamaanisha God Is Always With You…
Napenda kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu wangu na hii tattoo ni moja
kati ya vitu vinavyonikumbusha kuwa niko hapa duniani kwa sababu gani“>>>
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni