Kauli ya makamu wa rais, Ruto ameitoa akijibu hoja zinazotolewa na upinzani ambao unataka serikali kuachana na mpango huo na kwamba utachukua hatua za kisheria kupinga uamuzi wa Serikali, msimamo ambao naibu wa rais Ruto anasema serikali yake haitorudi nyuma wala kutishika.
Makamu wa rais William Ruto anasema kuwa ni kitendo cha kustaajabisha na kilichopitwa na wakati kuona viongozi wa upinzani wanatumia muda mwingi kutoa vitisho dhidi ya Serikali na kuongeza kuwa vitisho hivi havisaidii.
Makamu wa rais Ruto, aanatoa kauli hii wakati ambapo hii leo tume ya ardhi nchini humo inatarajiwa kuanza kutekeleza agizo la rais Uhuru Kenyatta kuchukua ardhi inayokadiriwa kufikia hekari laki 5ambayo ilikuwa inamilikiwa kinyume cha sheria.
-RFI
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni