GENN MEDIA

KANSAS COLLEGE OF NURSING

Jumamosi, 17 Januari 2015

Home » Ent. » Ni Mariah Carey na surprise hii kwa mashabiki wake Las Vegas…

Maria Carey

Huu ni ubunifu ambao hata mimi umenivutia, nakumbuka mwaka 2012 rapper Jay Z aliwahi pia kusurprise kwa kuingia kwenye treni ya abiria halafu akaendelea na safari, huku aliyekaa naye kiti kimoja alikuwa bibi mzee ambaye hata hakujua kwamba amekaa na staa mkubwa duniani!
Mariah Carey naye amekuja na hii kwa fans wake Las Vegas, mashabiki wake walikuwa wakihojiwa ndani ya vyumba vya hoteli, wakaeleza namna ambavyo wanamkubali staa huyo, halafu ghafla mlango unagongwa na mtu ambaye anajitambulisha kuwa ni mhudumu wa hoteli, halafu wanapogeuka kumuangalia mhudumu wanakuta mhudumu huyo ni Mariah Carey mwenyewe!

Hii imenivutia, katika surprise hiyo fans wake hao walipata nafasi ya shavu la ticket za show yake ambayo ataifanya May 6 Las Vegas, Marekani.
“Hili ni tukio muhimu kwangu na tena nina imani mashabiki wangu wataifurahia hii kwa sababu naenda kufanya shoo  ambayo ni kama njia ya  kuiongoza  album yangu ambayo ni toleo la 18,  naamini watu wengine watafurahia  kwa sababu sijawahi kufanya hivi kabla“ — Mariah Carey.
Video na pichaz za surprise hiyo ziko hapa.

Mariah-Carey-Confirms-Las-Vegas-Residency-Ellen (1)

wpid-img_20150115_214249

MRY



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni