GENN MEDIA

KANSAS COLLEGE OF NURSING

Jumanne, 29 Julai 2014

PALESTINA IKO TAYARI KUSITISHA MAPIGANO


Uongozi wa Palestina umependekeza makubaliano ya saa ishirini na nne ya kusitisha mapigano dhidi yake na Israel.

Yasser Abed Rabbo wa chama cha PLO, Palestine Liberation Organisation amesema mpango huo umeungwa mkono na makundi muhimu likiwemo kundi la Hamas na la Islamic Jihad.

Hata hivyo mmoja wa maafisa wa Hamas Abu Zuhri amesema taarifa hiyo ya PLO haiwakilishi upande wa Hamas.

Mapema pendekezo la makubaliano ya kusitisha mapigano lililotangazwa, halikuweza kutekelezwa kwa kuwa hakuna upande wowote ulioweza kulitekeleza kwa kusitisha mapigano katika eneo la Gaza.

Bwana Rabbo amesema ujumbe wa pamoja unaoongozwa na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas utakwenda Cairo kuweka masharti ya kusitisha mapigano.

-BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni